UTANGULIZI
Kwa
kawaida kabisa, hapana mtu ambaye anapenda kusubiri. Kila mtu hutamani kila
anachokifanya au anachopanga kukifanya kifanyike ndani ya majira na wakati
aliopanga tena kwa haraka.
Ukienda
bombani kuchota maji, hautatamani ukute foleni, utatamani uchote na kuondoka,
ukienda bank kufanya aina yoyote ya malipo, hutafurahia kukuta foleni ambayo
itakufanya usubiri, ukienda kituo cha basi na basi lisipowasili katika muda
uliotarajia, utajisikia vibaya na kukasirika kwakuwa unatakiwa kusubiri,
unapopiga simu kwa rafiki yako, na ukakuta anaongea na simu nyingine na unatakiwa
kusubiri lazima utakasirika tuu, unapopiga simu ya huduma kwa wateja na ukakuta
mhudumu hapokei kwasababu anaongea na simu nyingine na unatakiwa kusubiri, ni
wazi tuu utakasirika.
Hii
yote ni kwasababu kusubiri ni jambo gumu sana lenye gharama ambalo mara
nyingine hupima na kujaribu kiwango cha kuamini cha mtu. Na kiwango cha kuamini
kinapopimwa au kujaribiwa, maana yake kiwango cha uwezekano wa kuwezekana au
kutowezekana kwa mambo yanayotarajiwa au kusubiriwa kinapimwa na kujaribiwa
pia.
“Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia
kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya!
Katufanyizie miungu itakayo kwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa
katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.”
KUTOKA 32:1
No comments:
Post a Comment