The Wait


UTANGULIZI
Kwa kawaida kabisa, hapana mtu ambaye anapenda kusubiri. Kila mtu hutamani kila anachokifanya au anachopanga kukifanya kifanyike ndani ya majira na wakati aliopanga tena kwa haraka.
Ukienda bombani kuchota maji, hautatamani ukute foleni, utatamani uchote na kuondoka, ukienda bank kufanya aina yoyote ya malipo, hutafurahia kukuta foleni ambayo itakufanya usubiri, ukienda kituo cha basi na basi lisipowasili katika muda uliotarajia, utajisikia vibaya na kukasirika kwakuwa unatakiwa kusubiri, unapopiga simu kwa rafiki yako, na ukakuta anaongea na simu nyingine na unatakiwa kusubiri lazima utakasirika tuu, unapopiga simu ya huduma kwa wateja na ukakuta mhudumu hapokei kwasababu anaongea na simu nyingine na unatakiwa kusubiri, ni wazi tuu utakasirika.
Hii yote ni kwasababu kusubiri ni jambo gumu sana lenye gharama ambalo mara nyingine hupima na kujaribu kiwango cha kuamini cha mtu. Na kiwango cha kuamini kinapopimwa au kujaribiwa, maana yake kiwango cha uwezekano wa kuwezekana au kutowezekana kwa mambo yanayotarajiwa au kusubiriwa kinapimwa na kujaribiwa pia.
“Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayo kwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.”

KUTOKA 32:1
Unknown
Unknown

This is a short biography of the post author. Maecenas nec odio et ante tincidunt tempus donec vitae sapien ut libero venenatis faucibus nullam quis ante maecenas nec odio et ante tincidunt tempus donec.

No comments:

Post a Comment