MAOMBI NA
UTII
Pastor Sam
Gripper
28th
January 2018
UTANGULIZI
Nilikuwa
katika kutafakari na ikanibidi nifike point ambayo natakiwa kukubali kuwa moja
kati ya mambo magumu sana ambayo wanafunzi wa Yesu walimwomba Yesu awafundishe
kuyafanya ni namna ya kuomba. Sijui nguvu gani nyuma iliyo wasukuma katika
kufanya hilo, lakini naweza kuhisi kuwa walihitaji kufundishwa namna
wanavyoweza kujipatia mahitaji yao kutoka kwa Mungu kama wanavyohitaji.
Lakini
jambo gumu sana ni jambo ambalo Yesu anawafundisha kuwa wanatakiwa kuomba na
kutegemea mahitaji yao kwa Mungu, sio kama wao wanavyohitaji lakini kama Mungu
apendavyo kuwapa. MATHAYO 6:10 “Mapenzi
yako yatimizwe, hapa duniani kama mbinguni”.
Hakuna
mahali pagumu sana na panapohitaji Imani ya kweli na uthabiti wa mahusiano kati
ya mtu na Mungu, kama mahali ambapo upo kwenye uhitaji, unajua ni nini
unakihitaji kwa huo uhitaji ulio nao, lakini unatakiwa umwache Mungu ambaye
kikawaida kabisa hayupo katika hali unayopitia, afanye sio kama wewe
unavyotaka, lakini kama yeye anavyotaka. Wasiwasi mkubwa unaozaliwa hapa ni,
“Je, anajua exactly nini nahitaji kwa hali hii na atafanya kama vile
ninavyohitaji?”
Katika
point hii, pana mtego sana. Ndipo Yakobo 4:3 inasema “Hata mwaomba, wala hampati, kwa sabababu mwaomba vibaya, ili mvitumie
kwa tamaa zenu”.
“Akaendelea
mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe
hiki kiniepuke, walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe”
MATHAYO 26:39
Narudia
kuandika tena, katika point hii panahitaji uthabiti na uimara wa mahusiano
binafsi kati ya mtu na Mungu kiasi ambacho mtu ataamini kuwa mapenzi ya Mungu
hata kama hayatakuwa sawa na uhitaji, bado ni sahihi na kamili kwa kusudi
alilonalo Mungu kwa mtu.
Hitaji
kuu la Yesu katika maandiko hayo, ni kutoka katika adhabu inayomkabili. Lakini,
mapenzi ya Mungu kuhusiana na hali hiyo husika ni tofauti kabisa, na kwasababu Yesu amekwisha omba kuwa Mungu
atende kama anavyotaka, hana budi kukubali na kupokea nini Mungu anataka
kifanyike kwa hali iliyo mbele yake.
Ni
mara chache sana (wala simaanishi haiwezekani), Mungu huwa anaweza kuruhusu
maombi yetu yabadilishe nia na mtazamo wake juu ya jambo flani. Na hufanya
hivyo kwa makusudi maalum na wakati maalum. Lakini mara zote, Mungu huhitaji
maombi yetu yawe katika msingi wa kufunua na kutafuta mapenzi yake kwetu na kwa
hali tunazopitia na sio kumshawishi atende nini sisi tunataka.
Tatizo la mwanadamu, ni kutokuamini kuwa
mapenzi ya Mungu yanaweza kukidhi uhitaji alionao. Na sio kwamba hamuamini
Mungu, lakini ni kwamba haamini kuwa katika hali ya uhitaji anayopitia, Mungu
pia anapita na yeye katika hali hiyo na lolote atakalo litenda ni jema sana.
“Kwa sababu
hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini wala miili
yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
Waangalieni ndege wa angani ya kwamba, hawapandi, wala hawavuni, wala
hawakusanyi ghalani. Na Baba yenu wa mbinguni, huwalisha hao. Ninyi je!, si
bora kupita hao?”
MATHAYO
6:25-26
Maandiko
haya hayamaanishi kuwa Mungu hataki tujishughulishe na wajibu wetu wa kila siku
katika maisha. Anataka sana, asichokitaka ni katika hatua ya kutimiza wajibu
wetu wowote, tuzitegemee akili zetu. Alipo mwambia Adam na Eva kuwa wasile
matunda ya mti wa maarifa, sio kwamba hakutaka wawe na maarifa, lakini alitaka
kwa utayari wao kutii, yeye (Mungu) awe chanzo cha maarifa kwao na mwanadamu
amtegemee yeye kwa maarifa ambayo hayakuwa na uovu ndani yake.
Kuwa
tayari mapenzi ya Mungu yatimizwe kama yeye atakavyo, kuna gharama. Na moja
kati ya gharama hizo ni utayari wa kutii nini Mungu kupitia mapenzi yake
anataka kifanyike.
MAANA YA UTII
Kwangu
mimi, utii ni zaidi ya kufanya ulichoagizwa kufanya au kuacha ulichokatazwa
kufanya. Utii unachukua maana zaidi ya hapo, na katika chapisho hili,
nitautafsiri utii kama mlango wa Mungu kudhihirisha mapenzi yake kwa mtu
aliyemwomba.
Tunapomuomba
Mungu, tunaomba mapenzi yake yadhihirishwe, lakini namna pekee ya Mungu
kudhihirisha mapenzi yake, ni sisi kuchukua hatua ya kuishi sawa na kutenda
sawa na anavyotaka. Katika maandiko hapo juu, tumeona Yesu akiomba kikombe cha
adhabu kimuepuke (hivi ni jinsi yeye alivyotaka), lakini aliacha Mungu
adhihirishe mapenzi yake katika hilo na hata mara baada ya Mungu kudhihirisha
mapenzi yake, alikuwa tayari kuyatii.
Watu
wengi hupenda kuomba (jambo ambalo kimsingi sio baya), lakini sio wote huwa
tayari kufuata maelekezo ambayo Mungu huwapa kama namna ya kupokea majibu yao.
Hivyo utii, ni jambo pekee ambalo litamruhusu Mungu kudhihirisha mapenzi yake
kwa utayari wa mhusika kukubali na kutenda nini ataamriwa atende.
MAMBO
MAKUBWA MAWILI YANAYOPIMA KIWANGO CHA UTII CHA MTU
Jambo
la kwanza ni Mambo unayoyapenda au
kuyafurahia kufanya, na pili ni mambo
usiyoyapenda na hufurahii kuyafanya. Sio mara zote tunapomuomba Mungu, huwa
anajibu katika namna tunayoipenda au kuifurahia au sio kila mara zote hutoa
majibu tunayoyapenda. Waala simaanishi Mungu hajui nini tunahitaji na wala
hawezi kufanya sawa na tunavyohitaji. Lakini mara nyingine, mapenzi yake huwa
ni bora sana katika macho yake mwenyewe kuliko shauku zetu.
“Lakini yeye
akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je!
Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate mabaya? Katika mambo hayo yote
Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.”
AYUBU 2:10
Kiwango
cha utii wa mtu, huanza kupimwa katika eneo kama hili. Mahali ambapo uliyotarajia kuyapata kutoka kwa
Mungu ambayo kimsingi unayapenda na kuyafuahia ni tofauti na yaliyokuja, na
unatakiwa uyakubali na uyaishi pamoja na kwamba yamekuja katika namna ambayo
hukuitarajia au huifurahii.
Utii
wetu hauhesabiwi peke yake kwa kufanya mambo tunayoyapenda, lakini kama
utakutana na mambo usiyoyapenda na ukatakiwa uyakubali kwasababu ni mapenzi ya
Mungu kwako, utakuwa tayari kuyafanya?
Ukweli
wa msingi sana kuhusu mambo tunayoyapenda au kuyafurahia, ni kwamba
huturidhisha na kutufanya tujione tupo mahali flani ambapo tulitakiwa kuwa.
Ukiwa na rafiki ambaye anakupenda na kukufurahia, sio mara zote ataweza
kukwambia ukweli utakaokuuma, maana anajali kuhusu wewe na anaogopa kukuumiza.
Hivyo kwa namna hiyo, utajiona ni mkamilifu na huna haja ya kutia bidii katika
kuwa mtu bora zaidi maana hapana mtu anayezinyoshea vidole kasoro zako.
Ni
lazima mara nyingine kwasababu tuu tumeomba mapenzi ya Mungu yadhihirike, tuwe
tayari kutii na kuamini kuwa chochote alichokidhihirisha na kukileta kwetu kama
majibu ya maombi yetu, ni chema sana. Si tuu tufurahi kupokea mambo
tunayoyafurahia, lakini pia hata tusiyoyafurahia.
Tunafahamu
kuwa Ibrahim alikuwa akimsubiri Isaka kama ahadi ya Mungu kwa muda mrefu sana.
Na miaka michache mara baada ya Mungu kumpa majibu yake, Mungu akahitaji tena
Ibrahim amtoe Isaka (mwana wa pekee). Hii ilikuwa ni namna ya Mungu kupima utii
wa Ibrahim kwa kugusa kitu ambacho Ibrahim anakipenda na kukifurahia.
Hatutatii
hadi tutakapo kubali kuyaacha mambo tunayoyafurahia na kuyapenda kwa shauku
zetu, ili tutimize mapenzi ya Mungu na pale tutakapo takiwa kukubali kutii juu
ya mambo tusiyopenda wala kuyafurahia kwaajili ya mapenzi ya Mugu.
UTII HUFUNUA
:-
1.
Kibali
“Bwana
akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa
asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, name nitakupeleka kwa
Yese, Mbethlehemi, maana nimejipatia mfalme katika wanawe.”
1SAM 16:1
Jambo
pekee lililofanya Mungu ahamishe kibali kutoka kwa Sauli na kukipeleka kwa
Daudi, ni tendo la Sauli kukosa utii. Mungu alipomtuma Sauli akawaangamize
Waamaleki, alienda na kuangamiza vitu na watu ambao hakuwapenda wala kuwafurahia machoni pake lakini Mfalme Agagi na
mifugo mingine ambayo ilipata kibali machoni pake aliiacha hai. Utii wetu unapimwa kwa kukubali kuviharibu
hata vitu tunavyovipenda kwaajili ya mapenzi ya Bwana.
Kwa
kukosa kutii, Roho ya Bwana ilimwacha Sauli, na ninataka kuamini kuwa kwa tendo
hili, hakuna maombi ya Sauli ambayo yangepata kibali maalum sana mbele za Mungu
kama yalivyokuwa mengine yakipata kibali kabla hajamkosea Mungu. Hivyo kwa
kutii Neno la Mungu, tunapata kibali cha kukubalika machoni pa watu, lakini
zaidi machoni pa Bwana. Nimeandika lakini zaidi machoni pa Bwana, maana kuna
nyakati kutii kwako mapenzi ya Mungu kunaweza kukukoseshe kibali machoni pa watu
lakini kwa Bwana kitabaki vilevile.
2.
MAMLAKA
“Kama
mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi”
ISAYA 1:19
Siri
ya mamlaka na nguvu ya utawala, imefungwa katika tendo la utii. Unapokosa
kuyatii mapenzi ya Mungu na kufanya kinyume akuagizavyo, unapoteza nguvu ya
mamlaka na utawala na kumpa shetani nguvu hii juu yako. Katika hali ya namna
hiyo, hapana maombi utaomba maana u mtumwa, mtu asiyejua thamani na nguvu yake
katika ufalme wa Mungu.
Mathayo
4:1-11, Yesu kama Adam wa pili, hakuweza kuipoteza mamlaka yake kiurahisi
tofauti na Adam wa kwanza alivyotenda, kwasababu alisimama katika utii wa nini
mapenzi ya Mungu yanataka afanye. Na kwa namna hiyo, aliweza kuitunza mamlaka
na kwa sababu ya utii huu inakuwa ni rahisi na sisi kuipokea hii mamlaka
kwasababu hakukubali kuipoteza kwa kukosa kutii nini Neno la Mungu lilikuwa likimuagiza.
Kati
ya vitu vyote tunavyotakiwa kuviangalia kwa umakiini sana ili maombi yetu
yajibiwe kikamilifu, ni suala zima la kutii.
©
Pastor Sam Gripper 2018
#Betransfomed
No comments:
Post a Comment