WITO WA
MUNGU
GOD’S
CALLING
PASTOR SAM
GRIPPER
11th
Feb 2018
UTANGULIZI
Tuliumbwa
kwa kusudi ili tuweze kulitimiza kusudi. Na kama namna ya kutimiza kusudi la
kuumbwa kwetu Mungu hutupa njia za namna ya kuenenda katika kusudi ili
kulitimiza.
“Kila mmoja aliyeitwa
kwa jina langu, niliyemuumba kwaajili ya utukufu wangu, mimi nimwemumba, naam
nimemfanya”
ISAYA 43:7
Hivyo,
kusudi kuu ni kumtukuza Mungu. Na namna kuu ya kuliishi na kulitimiza kusudi
hilo ni kwa njia ya kuutumikia WITO WA MUNGU. Huwezi kufikia utimilifu wa
kusudi la Mungu pasipo kutembea ndani ya wito. Kusudi ni hatma (destination) na
wito ni barabara kuelekea hatma. Wote tunalokusudi moja (kumtukuza Mungu
kupitia maisha yetu), lakini njia za kulifikia kusudi hilo (Wito) huweza kuwa
tofauti.
“Ndani yake
tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa (tukiitwa) tangu awali, sawasawa na kusudi lake”
EFESO 1:11
KUSUDI -
> WITO - > HUDUMA - > KARAMA/VIPAWA/VIPAJI
Kwa
mujibu wa Waefeso 1:11, ni wazi kuwa kuitwa kwetu ni kwasababu ya kusudi ambalo
tunatakiwa kulitimiza. Na mfululio huo hapo juu, unaoesha kuwa ili tuweze
kufikia Kusudi tunahitaji Wito na Wito unatimizwa kupitia Huduma na Huduma
hutimizwa kwa kuvitumia vipaji, karama na vipawa.
Anaandika
Pastor Jimmy & Caroline Murphy katika kitabu chake cha Manabii na unabii katika kanisa
la leo, sura ya 6 kuwa huduma na karama au vipaji, ni sawa na fundi
seremala na box lake la vitendea kazi. Fundi seremala ni mhudumu anayetoa
huduma, lakini huduma yake haiwezi kulifikia kusudi husika, pasipo matumizi ya
zana za kazi ambazo ni karama, vipawa na vipaji.
Kama
lipo kosa ambalo vijana wengi, nikiwemo na mimi hulifanya, ni kudhani kuwa kila
mahali Mungu anapokuita (anapodhihirisha wito wake kwako), ni kwamba
anakupeleka katika kutumika katika zile huduma za ualimu, unabii, uchungaji nk.
Jambo ambalo wengi ndio hutafsiri kuwa ni maana ya wito.
Lakini nina uhakika kuwa Mungu anaweza
akakuita na kukupaka mafuta pia kumtumikia kwa kipaji ulicho nacho. Uchoraji,
uchongaji, ususi, upambaji, uandishi, uigizaji nk. Mungu alipomuumba Adam na
kumuweka katika bustani ya Edeni, alitegeea Adam atumike sio kama mchungaji,
mwanamaombi , nabii au muinjilisti, lakini alitakiwa kutumika kama Mkulima.
Hivyo
wito wa Mungu ka mtu ni mpana tofauti na wengi tulivyokuwa tunadhani ma ana lengo
la wito wa Mungu kwa mtu, ni kumleta mtu katika point ambayo atatumia yote
aliyonayo (vipaji na karama) ili kulitimiza kusudi la kuumbwa kwake ambalo ni
kumtukuza Mungu.
MAANA YA
WITO
Neno
Wito linatokana na tendo kuita au kutamka jina. Na kimsingi kutamka jina (to
name) ni zaidi ya kukitambua kitu (identifying/labeling). Kutamka jina ni
kukifanya kitu kiwe (to call something into being/ to make).
“Mungu
akasema iwe nuru, ikawa nuru. Akaiita nuru mchana na giza akaliita usiku”
MWANZO 1:3
“Bwana Mungu
akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani,
akamletea Adamu ili aone atawaitaje, kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu
likawa ndilo jina lake.”
MWANZO 2:19
Maandiko
haya mawili, yanaweza yakanisaidia sana kuielezea tofauti iliopo kati ya kuita
na kukitambua kitu. Mwanzo 1:3, inaonesha jambo ambalo kimsingi ndiyo msingi wa
kuitwa kwetu. Nuru haikuwepo hapo awali. Lakini Mungu anaifanya nuru iwe kwa
kuiita. Hivyo nuru inatokea katika hali ya utupu na inakuwa dhahiri kwakuwa tuu
Mungu ameiita.
Mwanzo
2:19, Mungu anaviumba viumbe, ndege na wanyama ambao kimsingi havikuwepo na
kuvileta katika hali ya kuwa, na baada ya kuwa anampa Adamu kazi ya kuvitambua
(identifying/labeling) viumbe hivi kwa majina.
Hivyo
msingi wa wito ambao Mungu anatuita, ni kuitwa kutoka katika hali ya upweke na
utupu na kuletwa katika hali ya kuwa ili tulifikie kusudi lake. Ni katika hali
hii Mugu huwa anatuita sio kwaajili ya kutumia tuu tulivyo navyo, lakini zaidi
kuviumba vitu vipya ndani yetu ili tuvitumie kwaajili ya kazi yake.
AINA KUU 2
ZA WITO
1.
Wito ambao
wanadamu sote tumeitiwa, kuwa wabeba sura ya Mungu
Kama
tulivyotangulia kuangalia hapo juu, kuwa msingi wa kwanza wa wito wetu ni
kuletwa katika hali ya kuwa (being) na aliyetuita ambaye ni muubaji wetu
(Mungu). Na ndio hasa jambo muhimu ambalo Isaya amelizungumza katika Isaya 43:7
kwamba tumeumbwa na kuitwa ili kulitimiza kusudi la Muumba.
Tumeumbwa
(tumeitwa) ili kumuakisi muumba katika maisha tutakayoyaishi na kupitia maisha
hayo, tutafikia kusudi kuu la kuumbwa kwetu ambalo ni kumtukuza Mungu.
Tunatakiwa kuishi kwa kumuakisi Mungu kwakuwa, sura ya Mungu kwa mtu sio
physical structure lakini ni spiritual structure.
Sura
ya Mungu kwa mtu, ni uwakilishi (divine presentation) anaokirimiwa mwanadamu
ili kumwakilisha Mungu katika maisha yake yote ya ulimwengu wa mwili.
MAMBO MAKUU
5 YANAYOELEZA SURA YA MUNGU KWA MTU
a. Asili ya
mwanadamu
Mwanadamu
ni muunganiko wa roho na mwili jambo linalompa maisha katika ulimwengu wa roho
na mwili pia. Katika ulimwengu wa roho, anachukua asili ya Mungu (Yohana 4:24),
katika ulimwengu wa mwili anaishi kama balozi na hekalu la Mungu (1KOR 6:19)
b. Utashi na
dhamiri
Utashi
ni uwezo lakini zaidi uhuru wa kufanya machaguo na maamuzi mbalimbali. Hii ndio
sababu ambayo ilifanya kwamba pamoja na Mungu kujua kuwa Adamu atakuja
kumkosea, lakini bado hakumzuia juu ya jambo hilo mbele yake, maana alimkirimia
utashi.
Lakini
pia utashi ni uwezo wa kupima matokeo
kabla ya kuchukua hatua ya kulitenda jambo. Kama ambavyo Mungu anaweza
kuutazama mwisho wa jambo kabla ya mwanzo, ndivyo ambavyo mwanadamu anaweza
kupima matokeo ya jambo kabla halijafanyika. Mfanya biashara kabla hajaanza
kufanya biashara, huwa anakaa na kuipima kisha anachukua hatua juu ya
alichokiona. Kwasababu hii ni tabia ya Mungu ambayo ameiwekeza kama sura yake kwa mtu.
c. Dhamiri
Uwezo
wa Mungu kuufunua utakatifu wake kwa mtu ili kumfanya tu awe na muitikio sahihi
kwa maadili. Mungu anamuumbia mtu dhamiri ili imuongoze katika maamuzi na
machaguo anayoyafanya na kumleta mtu katika point ya kuwa mtakatifu kama yeye
Mungu alivyo mtakatifu.
d. Uwezo wa
kuumba (Ubunifu)
Kila
tunapofanya kazi ya uundaji, tunaakisi uungu wa Mungu. Hivyo hii ni sura ya
Mungu aliyoiwekeza kwa mtu
e. Uwezo wa
kuhusiana
“Kila mmoja
kwa kadri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa
neema mbalimbali za Mungu”
1PETRO 4:10
Hili
ni jambo lingine ambalo linaelezea sura ya Mungu kwa mtu. Uwezo wa kuhusiana,
unafanya vipawa na karama ziwe rahisi kuhudumiana na kufaidishana. Kati ya
mambo yote mema ambayo Mungu aliyafanya katika bustani ya Edeni, ni jambo moja
tuu halikuwa jema machoni pake yeye mwenyewe.
Na jambo hili ni mtu kuwa peke yake. Sura ya
Mungu kwa mtu ni upendo, na ndio maana huwezi ukampenda Mungu usiyemuona wakati
mtu unayetakiwa kuhusiana naye hujampenda.
Hivyo,
wito wetu wa kwanza ni kuwa wmeba sura na mfano wa Mungu, jambo ambalo kila
aliyeitwa na Mungu (kutoka hali ya ktokuwepo na kuletwa hali ya kuwa)
anaushiriki.
2.
Wito ambao
unawahusu wateule
“Kwa maana
waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”
MATHAYO
22:14
Aina
hii ya pili ya wito ni msingi wa maisha ya mwamini ambayo yana tokana na
mwitikio wa kazi ambayo Mungu ameiweka ndani yake. Ni kweli, sote tumeitwa, kwa
maana ya kuumbwa kutoka katika utupu hadi kuwa hivi tulivyo, lakini si kweli
kwamba sote tumeteuliwa kuifanya kazi ambayo Mungu ameikusudia kwa wito wetu wa
pili.
“Alikuja
kwake, wala walio wake hawakumpokea. Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa
kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.”
YOHANA
1:11-12
Hivyo,
wito wetu mkuu kama familia inayoshiriki neema ya wokovu wa Mungu, ni kurejesha
sura ya Mungu kwa mtu iliyopotezwa kwa sababu ya uovu
“Basi Yesu
akawaambia tena, Amani iwe kwenu, kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami
nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho
Mtakatifu. Wowote mtakao waondolea dhambi, wameondolewa, na wowote mtakao
wafungia dhambi, wamefungiwa”
YOHANA
20:21-23
Kama
Mungu alivyofanya katika Mwanzo 2:7 kupuliza pumzi yake ya uhai puani mwa
mwanadamu mara baada ya kumuita, ndivyo ambavyo Yesu anafanya katika andiko
hili. Mara baada ya kufufuka, anawaumba wanafunzi wake kwa upya na kuwatiisha katika
mamlaka ya utawala kama Makristo hapa duniani. Anawapulizia pumzi yake ya uhai,
na kupitia pimzi hiyo anawapa Roho Mtakatifu (anafanya uumbaji wa pili) na
kuwapa mamlaka ya kusamehe kwa niaba ya Mungu.
Huu
ni wito wetu wa pili ambao tumeitiwa. Mara baada ya anguko la mwanadamu, sura
ya Mungu kwake ilifutika na kuliathiri kusudi la Mungu kwake. Hivyo mwanadamu
katika kutenda, akawa hawezi tena kutenda kwa kutegemea utashi na ufahamu wake
ili kumpendeza Mungu kama ilivyokusudi la kuumbwa kwake. Hivyo kwa nana yoyote,
lazima sura ya Mungu kwa mtu irejeshwe. Na Roho Mtakatifu kupitia sisi, ndio
anaifanya hiyo kazi kila mara tunapowafikia watu walio gizani.
“Kila mtu
aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake.
Wala hawezi kutenda dhambi kwasababu amezaliwa kutokana na Mungu.” Katika hili,
watoto wa Mungu ni dhahiri na watoto wa ibilisi nao. Mtu yeyote asiyetenda haki
hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake”
1YOHANA
3:9-10
Hii
ndio kazi ya pili tuliyoitiwa ili kuwafanya
watu wasiomjua Mungu warudi katika kuwa wabeba sura ya Mungu. Hili halihitaji
uwe muhubiri, mwimbaji, muinjilisti, mwalimu nk. Hizo ni huduma tuu za kuuishi
na kuutimiza wito kama ambavyo unaweza kuwa muuza nyanya na kupitia kazi yako,
watu wakaokolewa.
“Vivyo
hivyo, nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema,
wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”
MATHAYO 5:16
ILI KUTAMBUA
WITO NA POSITION AMBAYO UNATAKIWA KUWA ILI KUUTUMIKIA WITO WAKO UNATAKIWA
KUFANYAJE?
Hili
ni swali ambalo rafiki yangu mmoja aliwahi kuniuliza. “Nawezaje kuutambua wito
wangu au mahali ambapo natakiwa nisimame ili kuutimiza? Natakiwa kwanza niwe
mchungaji ili kuutimiza au?”
Kama
nilivyotangulia kuandika hapo awali. Watu wengi na mimi nikiwepo, tumekuwa
tukilichukia sana hili neno wito wa Mungu kwakuwa, tumewaza kuwa kila mara
Mungu anapofunua wito wake kwetu, ni lazima atuchukue na kutupeleka katika
uchungaji, uinjilisti, ualimu nk hata kama hatupendi. Nakubali na ninayatambua
mazingira ambayo Mungu aliwahi kuwaita watu katika maeneo nyeti sana ya
kiutumishi hata kama hawakupenda kutumika huko. Lakini ni kwa makusudi na
nyakati maalu, Sio mara zote Mungu hufanya hivyo.
Unahitaji
kuwa na Roho Mtakatifu
“Yeye
atanitukuza mimi; kwakuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari”
YOHANA 16:14
Roho
kwa kuyatwaa yaliyo ya Mungu na kutupasha habari, huzifanya upya fahamu zetu
ili tuyajue mapenzi ya Mungu kwetu ni yapi. Tendo la kuyajua mapenzi ya Mungu
hutupa muitikio sahihi juu ya nini Mungu anataka tufanye. Hili hutusaidia kukaa katika position ambayo
yeye Mungu amekusudia kwaajili ya kutuwezesha kutembea ndani ya wito huu mkuu
tulio teuliwa kuufanya.
Roho
ndio hutoa karama na vipaji na humassign mtu mahali ambapo yeye Roho ameona mtu
huyo tafaa kuwepo hapo. Hivyo, pasipo Roho Mtakatifu, ni ngumu sana kujua ni
wapi unatakiwa kukaa ili kuutimiza wito wako. Roho Mtakatifu yupo tayari
kukusaidia, unachotakiwa kufanya ni kuwa tayari kumpoea na kuruhusu badiliko
kamili ndani yako.
1 WAKORINTO
12:28, WAEFESO 4:11, WARUMI 12:6-8
Mara
baada ya kujua karama na kipawa chako, hakikisha huchi kukichochea. Tumia mara
nyingi kadri uwezavyo pasipo kujali lolote. Hiyo ni namna ya wito ulioitiwa na
utadaiwa kama utashindwa kutenda kwa bidii.
BE
TRANSFORMED!
©By
Pastor Sam Gripper
TAG PENUEL LUHANGA & TOTAL
TRANSFORMATION YOUTH MINISTRY
0657670972
No comments:
Post a Comment