KUSHUGHULIKA NA MTAZAMO



KUSHUGHULIKA NA MTAZAMO

4th February 2018

By Pastor Sam Gripper



MAANA YA MTAZAMO

Ni mwenendo, tabia au muitikio wa mtu juu ya jambo flani, ni namna jambo linavyotazamwa na kuonwa kiujumla. Sote tunaweza kufanana katika namna ya maumbile, lugha, asili na mambo mengine kama hayo, lakini sio kweli kwamba sote tunaweza kuwa na mtazamo sawa.

Msingi wa tofauti zetu huanzia katika point hii ndogo na isiyoonekana. Mawazo yako, muitikio wako juu ya jambo fulani, namna unavyofanya maamuzi na kupima mambo mbalimbali, ndiyo hasa hutafsiri wewe ni nani, lakini zaidi hukutofautisha na wengine.

KWELI KUU 3  KUHUSU MTAZAMO NA MUITIKIO WAKO JUU YA JAMBO

Ukweli wa kwanza, vitu vingi vinavyokatishaga au kuzuia safari zetu huwa sio matatizo wala haviji kama matatizo, lakini shauku yetu (nguvu inayotusukuma juu ya mambo tunayotarajia), mtazamo na muitikio wetu juu ya mambo kama hayo, ndiyo hasa huvifanya vitu hivyo vionekane kama tatizo au vizuizi vya sisi kuendelea.

“Bwana akamwambia Musa, mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israel waendelee mbele. Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya, nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu”

KUTOKA 14:15-16

Jambo ninalotaka tulitazame hapa ili pia linisaidie katika kuielezea point yangu ya kwanza ni kwamba, asilimia kubwa ya mambo yanayotuzuia sio matatizo na hayaji kwetu kama matatizo. Historia zetu, shauku zetu, muitikio na mitazamo yetu ndiyo hasa hufanya mambo haya yawe matatizo.

Mwanzo 1:31, inaposema Mungu alikiona kuwa kila alichokiumba ni kamilifu na chema, kati ya hivyo ilikuwemo pia Bahari ya Sham. Na alipokuwa anaiumba, hakuwa analiumba tatizo wala zuio la Wana wa Israeli kutoka Misri. Hivyo bahari haikuwa tatizo. Nataka kuamini kuwa zilikuwepo shughuli nyingi tuu za kiuchumi zilizokuwa zinategemea uwepo wa bahari hii na wafanyaji wa shughuli hizo, waliichukulia na kuitazama bahari kama fursa kwao na sio zuio au tatizo.

Lakini historia ya wana wa Israel, shauku waliyokuwa nayo ya kutoka mikononi mwa watesi wao, mitazamo na muitiko wao walipokutana na bahari ile ndiyo hasa vilifanya ionekane kama tatizo na zuio la safari yao, lakini katika namna halisi ya uumbaji, bahari ya Sham haikuwa tatizo.

Na ndio maana mara baada ya Mungu kuwapa “mtazamo wake” kwamba hata bahari inaweza kuwa njia na kuwavusha, hakuiacha iendelee kuwa njia kwa wengine kwasababu hakuiumba ili iwe njia ila iwe bahari, na akairudisha kama ilivyokuwa kwasababu ilikuwa ni zuio kwa wana wa Israel tuu, lakini kwa wengine ilikuwa ni fursa. Hivyo kama Mungu angeiacha iendelee kuwa njia, angekuwa ameziharibu fursa za watu wengine waliokuwa wakiitegemea bahari ile ili kuendesha maisha yao.

Nataka kuzungumza nini hapa? Ni hivi, yapo baadhi ya mambo ambayo kimsingi yaliumbwa kuwepo na yalitakiwa yawepo katika maisha ya kila siku. Lakini shauku yetu ya kufika mahali, mitazamo na miitikio juu ya mambo kama hayo, vinaweza kutuambia kuwa mambo hayo ni matatizo na vizuizi vya sisi kuendelea. Katika point kama hii, hatuwezi kuyavuka mambo kama hayo, pasipokujua mtazamo wa Mungu juu ya mambo hayo.

Wana wa Israel walipokutana na bahari, hawakuwa na haja ya kumwomba Mungu aikaushe. Na maandiko yanaeleza wazi kuwa hawakuwa na jambo la kufanya zaidi ya kumlaumu Musa. Mtazamo na muitikio wao kwa uwepo wa bahari ile ulikuwa ni kuiona ile bahari ni tatizo na zuio. Jambo kuu ambalo lilikuwa ni ukombozi kwao, lilikuwa ni kumsikiliza Mungu ana mtazamo gani juu ya hali iliyokuwa mbele yao ambayo kimsingi haikuwa tatizo kwa Mungu.

Hivyo, tunahitaji kuwa na akili, ufahamu na nia (mind) ya Kristo na mtazamo wake, tunapodeal na mitazamo yetu katika kutatua na mambo yanayotuzunguka.

“Basi mwanadamu wa tabia ya siri, hayapokei mambo ya Roho wa Mungu maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwakuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.”

1WAKORINTHO 2:14-16

Nia ya Kristo ndani yetu, ndiyo hasa hushughulika na kuibadili mitazamo yetu. Sio mara zote mambo tunayokutana nayo huwa kama matatizo, lakini mitazamo yetu huweza kufanya yaonekane kama ni matatizo. Tunapokuwa na nia au ufahamu wa Kristo tunayatazma kama yeye ayatazamavyo.
Ukweli wa pili, Kikawaida mtazamo wa mtu huwa unaathiriwa sana na position aliopo. Kama utautazama Mlima Kilimanjaro ana kwa ana, ni mlima mrefu ambao kwa namna yoyote huwezi kuuvuka na kwenda upande mwingine. Lakini ukiutazama mlima huo huo kutokea juu, hutauona kwa urefu ambao uliuona ulipokuwa unautazama ana kwa ana. Utauona ni kama kidoti fulani tuu. Hii ni kwasababu, position yako imebadilika.




Kulingana na eneo/ mahali ulipo, kila unachokiona kina nafasi kubwa sana ya kukutafsiri na kuyatafsiri maisha yako kwa vile ulivyokiona, kulingana na mahali ulipo. Nuru na giza haviwezi kukubaliana juu ya kitu kimoja, na ndio maana maandiko yanatuambia kuwa hapana urafiki kati ya mtu wa giza na mtu wa nuru kwasababu ya utofauti wa position walizopo.

“Niyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu. Lakini Mungu kwakuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu.”

EFESO 2:1,4-6

Mstari wa kwanza wa kitabu cha Waefeso sura ya 2, unaanza kueleza juu ya position tulizokuwepo katika maisha yetu ya kale. Tulikuwa wafu kwasababu ya makosa na dhambi zetu. Kwa jinsi hii, ni wazi kwamba kuna namna mitazamo yetu iliathiriwa na position tulizokuwepo. Tulideal na mambo yanayotuzunguka kulingana na wapi tulipo. Lakini ashukuriwe Mungu ambaye kama namna ya kuanza kudeal na mitazamo yetu, alianza kubadilisha position tuliopo.

Mstari wa 4, unaanza kuelezea kuwa alituhuisha pamoja na Kristo, na mistari iliyobaki inasema, akatuketisha pamoja na Kristo katika ulimwengu war oho. Hivyo ni wazi kuwa, hatutakuwa tukiyaangalia mambo na kudeal nayo kama tulivyokuwa tukideal nayo tulipokuwa wafu kwasababu ya dhambi na makosa yetu, lakini tutayatazama na kudeal nayo kama Kristo anavyoyatazama maana tumeketishwa pamoja naye.

Ukweli wa tatu, mtazamo wako haumuathiri mtu mwingine yeyote isipokuwa wewe mwenyewe. Na hili ndilo jambo baya na hatari sana kuhusu mtazamo wa mtu. Wakati umeruhusu jambo flani lionekane ni tatiz kwako, jambo hilohilo kwa mwingine linaweza kuwa ni fursa ambayo itampelekea kufanya mageuzi makubwa ya hali yake husika.

Watu wote waliofanya ugunduzi mkubwa wa viombo vya usafiri, njia za mawasiliano na mambo kama hayo, hawakuruhusu kuona mambo yanayowazunguka kama matatizo, badala yake waliyaona kama fursa zinazowapelekea katika ugunduzi wao mkubwa. Na kwa upande mwingine, watu wote waliokubali kukata tamaa, ni watu ambao hawakutaka kubadlisha mitazamo yao juu ya mambo wanayokutana nayo.

Siri ya ukuu wa mtu inaanza katika namna anavyotumia mtazamo wake katika kushughulika na mambo yanayomzunguka. Mtazamo hasi, hauwezi kuona jema hata katikati ya mema, lakini mtazamo chanya huweza kuhesabu mema hata katikati ya mabaya. Sio matatizo yanayotukwamisha, lakini ni mitazamo yetu juu ya matatizo hutukwamisha. Badili mtazamo ili ubadili maisha.





© Pastor Sam Gripper

TAG PENUEL LUHANGA

#2018betransformed

TOTAL TRANSFORMATION
Unknown
Unknown

This is a short biography of the post author. Maecenas nec odio et ante tincidunt tempus donec vitae sapien ut libero venenatis faucibus nullam quis ante maecenas nec odio et ante tincidunt tempus donec.

No comments:

Post a Comment